HAPO MWANZO
HAPO MWANZO, Mungu aliziumba mbingu na nchi.
Unajua baada ya HAPO MWANZO kuziumba mbingu na nchi na kufanya uumbaji huo siku sita hakuumba tena?
Nikatafuta wakati wa HAPO MWANZO kama Mungu aliumba meli,magari,majiko ya gesi, pete za dhahabu,mashati,suruali,viatu sikuona.
Nikatafuta baada ya HAPO MWANZO kama Mungu alitengeneza mikoba kwa kutumia ngozi za wanyama, nikakosa.
Kwa nini ubaki kwenye HAPO MWANZO? Unajua nini kilitokea baada ya HAPO MWANZO? Baada ya HAPO MWANZO Mungu akaweka uwezo wa mwanadamu kuumba vitu. NUHU akatengeneza MELI ya kwanza kabla ya Archimedes kugundua kanuni ya kuzama na kuelea kwa vitu.
Edison Thompson akaumba Bulb baada ya Mungu kuitq giza usiku. Jr Dugilo akaandika kitabu cha Ongenza uwezo, Amina Sanga akaandika Nguvu ya uthubutu, Emmanuel Makwaya Godfrey akaandika To be is to do, James Kalekwa akaandika Iandike njozi yako. Mark akatengenza Facebook
Na wewe unajua kuwa Mungu aumbi kiti cha mbao, ukitaka kiti cha mbao nenda kwa fundi seremala.
Baada ya hapo mwanzo, Mungu amekasimisha uwezo wa kutengeneza batiki ndani ya Yohana Mwaigomole na vitu vyote ndani ya mwanadamu.
Hayo yote Mungu amekupa rasilimali inaitwa AKiLi na Roho Mtakatifu(msaidizi; hafanyi kazi mpaka uanze).
HAPO ULIPO is loading.......